Rubani wa kwanza wa kike Kenya Gaudentia Aura, aaga dunia

July 2024 ยท 2 minute read

- Guadentia Aura alikuwa mwanamitindo wa kimataifa na alifanya kazi na kampuni kadha

- Aura alikuwa Mwafrika pekee ambaye uso wake ulitumika katika bidhaa za urembo za Unilever

- Kando na taaluma yake ya urembo, Aura pia aliibuka rubani wa kwanza wa kike Kenya ambapo alihudumu katika mashirika mbali mbali ya Scandivania

Familia ya mwanamitindo wa zamani Gaudentia Aura imethibitisha kifo cha mrembo huyo.

Kulingana na dada yake marehemu Celestine, Aura alipumua pumzi yake ya mwisho mnamo Jumatatu, Februari 24 usiku.

Habari Nyingine: Kocha afutwa kazi kwa kuvua nguo kusherehekea ushindi dhidi ya klabu ya zamani

Habari Nyingine: Mwanahabari Eric Kabendera aachiliwa huru baada ya kuwa mahabusu miezi 6

Katika siku zake, marehemu alikuwa mwanamitindo wa kimataifa na alifanya kazi na kampuni kadha ikiwemo kampuni ya sabuni ya Lux.

Kando na taaluma yake ya urembo, Aura pia alifuzu katika nyanja tofauti na kuwacha historia ya kuwa rubani wa kwanza wa kike Kenya.

"Ni huzuni, nina maanisha ni huzuni sana ulienda kuwa na Mungu leo asubuhi. Nyoyo zetu zimeshindwa kukubali ukweli. Ni ndoto? Rubani wa kwanza wa kike Afrika, Miss Kenya,mwanamitindo, balozi wa Lux , mwerevu, malkia wa Kingereza," Celestine alithibitisha.

Habari Nyingine: Magazeti ya Kenya, Jumanne, Februari 25: Uhusiano wa karibu kati ya ofisi ya DCI na DPP wakatika

Jamaa na marafiki walimuomboleza kama mwanamke ambaye hakuwa na uwoga wa kufuata moyo wake katika nyanja tofauti.

"Ni huzuni kubwa kuwa ufalme wa Wanga unaomboleza kifo cha binti wao mpendwa Gaudentia Aura," aliandika Tobia Omono.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdjaX91fpJmqa6akaO2bsPAZqKwmZ6vrm7DwGaioqOVYq%2BivsBmmJ%2BqmaCubrPArpuepqSerm6t1KuYZpmRnK5usNSnoJpmmKm6rQ%3D%3D